Masheikh 9 ambao ni miongoni mwa wanaoshikiliwa kwa zaidi ya Miaka 10 katika Gereza Kuu la Kisongo wamesomewa Mashtaka katika Mahakama Kuu ya Kanda, ambapo 6 kati yao wamekutwa na hatia ya kulipua Kanisa Katoliki la Parokia ya Mtakatifu Joseph Olasiti Mwaka 2013, na kuhukumiwa kunyongwa.
![](https://jambofm.co.tz/wp-content/uploads/2023/12/487205d11c724fa06116bb8b6964a08f-1024x575.webp)
Katika hukumu hiyo Jaji alionesha kuridhishwa na ushahidi wa Polisi kwamba Masheikh hao akiwemo Imamu Mkuu wa Masjid Quba Sheikh Jaafar Hashim Lema walilipua Kanisa Katoliki na kusababisha madhara makubwa.