Categories

Do you have a Story?

Call us on 0677 644 444 to submit your news story or incident report!

Wanafunzi 17 walazwa hospitali  baada ya kula futari

Mwanafunzi wa Sekondari ya Kilolo mkoani Iringa amefariki  wengine 17 wamelazwa  katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo  baada ya kudaiwa kula chakula cha Msaada kilichotolewa kama Futari katika Msikiti wa Luganga

Afisa Afya wa Wilaya, Dkt. Fanuel Nyadwike amesema  tayari Sampuli zimechukuliwa na kupelekwa kwa Mkemia Mkuu na kinachosubiriwa ni majibu , na wanachokifanya kwa sasa  ni kuwapatia huduma wanafunzi  ambao wamelazwa.

Tukio hilo limeibua maswali kuhusu  msaada huo, na kuhoji ni watu wangapi walikula chakula na je, wote wamepata madhara?

Uongozi wa Shule haujapatikana kuongelea tukio hilo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *