Katika mwezi huu wa KU-ME ulioanza jana, staa wa muziki Beyoncé alihitimisha ziara yake ya ‘Renaissance World Tour’ ambayo iliyoanza kutimua vumbi Mei 10 mwaka huu jijini Stockholm nchini Sweden na kumalizika jana Oktoba mosi, jijini Kansas -Marekani.
Inaelezwa kuwa Beyonce amefanya jumla ya shoo zipatazo 56 ndani ya nchi12 kwenye miji zaidi ya 10 na waliofika kushuhudia shoo wanakadiriwa kufika zaidi ya Milioni 2, hapo achia mbali Blue Ivy fans eeh.
Na kwa sasa Queen B yupo kwenye mazungumzao ya mwisho na kampuni ya AMC kwaajili ya Filamu ya Tamasha la ‘RENAISSANCE’ na tayari ameachia trela ya filamu hiyo ambayo itaonyeshwa Desemba 1, mwaka huu.