WAZAZI NA WALEZI WATAKIWA KUWEKEZA ZAIDI KATIKA MALEZI YA WATOTO

Na Eunice Kanumba – Shinyanga.

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu, David Lyamongi amewataka wazazi na walezi kuwekeza kwa dhati katika malezi na makuzi ya watoto kuanzia wakiwa tumboni ilikuimarisha maadilina kuleta tija kwa taifa katika siku zijazo.

Lyatonga ametoa wito huo wakati  akifungua kongamano la maadhimisho ya siku ya kimataifa ya familia kwa mkoa wa Shinyanga kwa niaba ya katibu tawala mkoa wa Shinyanga lililofanyika katika ukumbi wa kalinjuna uliopo katika ofisi ya mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali na serikali  wakiongozwa na mganga mkuu wa mkoa wa Shinyanga Dr Yudas Ndugulile.

Viongozi wengine ni kutoka katika madhehebu ya dini,kamati ya Amani ya mkoa,wawakilishi wa baraza la wazee,baraza la watoto,vyama vya watu wenye ulemavu  wadau wa maendeleo,shirika la ICS,klabu ya waandishi wa habari,watalamu wa masuala ya kijamii wanafunzi kutoka vyuo na shule za sekondari ambapo kauli mbiu katika maadhimisho hayo  kwa mwaka 2025 ikisema “mtoto na malezi msingi wa familia bora na taifa imara”

“Niwatakie  wazazi na walezi wote mkoani Shinyanga  kuhakikisha wanawekeza ipasavyo katika malezi na makuzi ya watoto wetu  kuanzia wakiwa tumboni ili tuweze  kujenga taifa lenye  msingi imara maadili na maendeleo endelevu”amesema Lyamongi.

Awali akimkaribisha mgeni rasimi  mganga mkuu wa mkoa wa Shinyanga Dr Yudas Ndugile kongamano hilo lina lengo la kuwaleta pamoja wadau wote wa malezi ya watoto  kwa ajili ya kutafakari  na kubadilishana  uzoefu juu ya jitihada zinazofanywa  katika kuimarisha malezi na makuzi bora kwa watoto.

Kwa upande wake afisa ustawi wa jamii mkoa wa Shinyanga Lyidia Kwesigabo amebainisha kuwa kila mwaka may 15  Taanzania  huungana na mataifa  mengine duniani kuadhimisha siku kimataifa ya familia  ikiwa ni fursa ya kutathimini mchango wa jamii katika maendeleoya watoto na familia kwa ujumla.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *