Baraza Kuu la Umoja wa Vijana CCM ( UVCCM ) Taifa limeitaka Serikali kutoa majibu kwa Vijana ni lini mikopo ya 10% itarejeshwa baada ya kusitishwa kwa miezi kadhaa na kwamba limeipa Serikali siku 7 kutoa majibu na isipofanya hivyo basi Wizara husika zijitathmini kama zinatosha kusimamia maslahi ya Vijana.
![](https://jambofm.co.tz/wp-content/uploads/2024/01/87ca3601-ce60-4dc2-9621-b9bc173be865-1024x678.webp)
Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Mohammed Kawaida amesema hayo Mkoani Kigoma baada ya Baraza hilo kumaliza vikao vyake vilivyofanyika Mkoani humo na kutoka na maazimio hayo.