Categories

Do you have a Story?

Call us on 0677 644 444 to submit your news story or incident report!

T.I achukizwa na mtoto wake kumkataa Tupac

Rapa T.I achukizwa na kitendo cha kijana wake King Harris kutofahamu kuhusu rapa Tupac kuwahi kuwa muigizaji.

T.I alionesha kuchukizwa na hali hiyo wakati wa kipindi cha “GOAT Talk” kinachorushwa na Complex ambapo walikuwa na mazungumzo yaliyokuwa yakijadili ni rapa -mwigizaji gani wanavutiwa nao.

Ndipo King akasema kuwa hajua kuwa Tupac aliigiza katika filamu yoyote, ndipo T.I akamwambia King “ Toka nje! Ondoka.”

Wakati wanaendela kuongea ndipo King aliongeza, kuwa “Muigizaji anayempenda zaidi wa rap ni Ice Cube.” ..Ndipo wawili hao waliweza kukubaliana juu ya hilo.

Ila King akachafua hali ya hewa kwa kusema mwingine ni Will Smith, T.I. akabaki anashangaaa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *