Categories

Do you have a Story?

Call us on 0677 644 444 to submit your news story or incident report!

RC Mndeme akaa kikao na Wadu wa michezo Stand United FC

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe Christina Mndeme, mapema leo ameongoza kikao cha wadau wa michezo wa mkoa wa Shinyanga, kujadili na kutafuta suluhu ya kuikomboa kiuchumi klabu ya Stand United FC inayoshiriki ligi ya Championship Tanzania.

Pamoja na mambo mengine kikao hicho kimeazimia kuunda kamati ya watu sita (6), itakayokuwa na jukumu la kuweka mipango mikakati ya kutafuta wadhamini na wadau mbalimbali wa kuisapoti timu hiyo, ili kufikia lengo lake la kucheza ligi kuu.

Pia katika kikao hicho, kiasi Cha shilingi Milioni 8.74 zimechangwa, ambazo kati ya hizo pesa ya mkononi (cash) ni Milioni 1.66, ahadi ni Milioni 7.80, ambazo zimekabidhiwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi kwa niaba ya kamati hiyo iliyoundwa leo.

Aidha Mkuu wa Mkoa Mhe. Mndeme ameipongeza na kuishukuru kampuni ya Jambo Food Products kwa kuisaidia timu hiyo kwa kipindi kirefu, huku akiwataka wadau na makampuni mengine kushirikiana nayo katika kuisaidia Stand United FC.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *