Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan ameongeza siku saba mbele kuendelea kwa maonyesho ya Wakulima nane nane kimataifa katika viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya.
Hatua hiyo inakuja baada ya Mbunge wa Jimbo la Mbeya ambaye pia ni Spika wa Bunge la Tanzania Dkt. Tulia Ackson kuomba maonyesho hayo yaongezwe muda kwa siku saba kutokana na maboresho yanayotarajiwa kufanywa katika eneo hilo la maonyesho.