Muigizaji kutoka Nigeria, Regina Daniels ameweka wazi ni bora ampatie figo mumewe ambaye ni mwanasiasa Mh. Ned Nwoko, kuliko baba yake mzazi.

Mrembo huyo amefunguka hayo kwenye mahojiano ya hivi karibuni, wakati wa uzinduzi wa filamu yake mpya iitwayo ‘Switching Places’, na kubainisha kuwa atafanya hivyo kwani atakuwa anaokoa watoto wake aliyozaa na kiongozi huyo.