Mwandishi wa habari Congo, hatiani kwa kueneza habari za uongo

Mahakama nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imemhukumu kwenda jela miezi sita mwandishi wa habari wa nchini humo, Stanis Bujakera baada ya kumtia hatiani kwa kueneza habari za uongo.



Mbali na adhabu hiyo, mwanahabari huyo ambaye anafanya kazi katika vyombo vya habari vya kimataifa ikiwa ni pamoja na jarida la Jeune Afrique na Reuters ameamuriwa kulipa faini ya TZS 928,000.

Bujakera, ambaye alikana mashtaka yote, alikamatwa katika mji mkuu Kinshasa kwa tuhuma za kueneza habari za uongo kuhusu mauaji ya mwanasiasa mashuhuri wa upinzani, katika makala iliyochapishwa na Jeune Afrique, gazeti la habari la Ufaransa limesema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *