Categories

Do you have a Story?

Call us on 0677 644 444 to submit your news story or incident report!

Jay Jay Okocha waziri mpya wa michezo Nigeria

Rais wa Nigeria, Bola Tinubu amemteua mshambuliaji wa zamani wa PSG na timu ya Taifa Nigeria, Augustine Azuka Okocha almaarufu ‘Jay Jay Okocha’ kuwa Waziri wa Michezo, Vijana na Maendeleo.

Okocha (46) amewahi kuvitumikia vilabu vya Eintracht Frankfurt, Fenerbahçe na Bolton aliichezea timu ya Taifa Nigeria mechi 73 huku akipachika magoli 14 kati ya mwaka 1993 na 2006.

Okocha ambaye alijulikana uwanjani kwa kupiga chenga za maudhi na uhodari wa upigaji wa mipira iliyokufa, alitwaa medali ya dhahabu katika michuano ya Olympic 1996 na kombe la AFCON 1994 sambamba na tuzo ya mchezaji bora wa michuano ya AFCON 2004.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *