Categories

Do you have a Story?

Call us on 0677 644 444 to submit your news story or incident report!

Yanga yaangukia pua rufaa ya adhabu ya Khalid Aucho

Kamati ya usimamizi na uendeshaji wa Ligi Kuu Tanzania bara (TPLB) imetupilia mbali rufaa ya klabu ya Yanga ya kutaka marejeo (review) ya adhabu ya kiungo wake Khalid Aucho ambaye amefungiwa michezo 3 na faini ya Tsh laki tano (500,000) kwa kosa la kumpiga kiwiko kiungo wa Coastal Union Ibrahim Ajibu kwenye mchezo uliochezwa Novemba 08, 2023.

Baada ya kupitia shauri la Yanga na kanuni za Ligi, Kamati ya TPLB imejiridhisha kwa mara nyingine kuwa adhabu iliyotolewa kwa mchezaji huyo ni sahihi hivyo anapaswa kuendelea kuitumikia, huku ikimtaka mchezaji huyo kuzingatia mchezo wa kiungwana wakati wote.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *