Sunna Sepetu, dada wa Miss Tanziania 2006 Wema Sepetu ambaye anaishi Worcester, Massachusetts, amepatikana na hatia ya utakatishaji fedha nchini Marekani, atahukumiwa kifungo cha miaka 20 jela.
Sunna(37), na mwenzake Nafise Quaye (47) wa Nigeria walitumiwa kufanya Miamala kwa njia ya Mtandao kati ya mwaka 2013 hadi 2019 takriban dola milioni 3.2 ambazo ni zaidi ya TZS bilioni 8.
Hakimu wa Mahakama huko Concord, Massachusetts, Samantha Elliot baada ya kesi ya siku nane Mahakamani amedai hukumu imepangwa kutolewa kwa washtakiwa wote wawili Julai 8, 2024.