Na Clavery Christian – BUKOBA.
Katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika, Shirika la TEKLA limefanya tukio maalum la kugawa msaada wa vifaa kwa watoto wenye ulemavu mkoani Kagera, kama ishara ya upendo, kuwajali na kuwathamini.
Mkuu wa Wilaya ya Missenyi, Kanali Mstaafu Hamis Maiga aliyekuwa Mgeni Rasmi, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kagera aliipongeza TEKLA kwa mchango wake mkubwa kwa jamii, akisema kuwa hatua hiyo ni ya kupongezwa na inapaswa kuungwa mkono na mashirika me wa binadamu. Hii ni njia ya kuonesha kuwa kila mtoto anathaminiwa, anastangine.

“Kuwajali watoto wenye ulemavu ni kuenzi utuhili fursa sawa, na ni sehemu ya maendeleo ya taifa letu,” alisema DC Maiga
Mkurugenzi wa TEKLA, Annalise Leonard Lubago alisema kuwa shughuli hiyo inalenga kutoa hamasa ya upendo na mshikamano kwa watoto waliopo katika mazingira magumu, hasa kipindi hiki cha kuelekea Juni 16 – Siku ya Mtoto wa Afrika.
“Watoto hawa wanahitaji mazingira rafiki, msaada wa vifaa na sauti ya matumaini. Tunayo dhamira ya kuona hawabaki nyuma katika safari ya maendeleo,” alisisitiza Annalise Mkurugenzi wa TEKLA.

Wazazi na walezi wa watoto walionufaika na msaada huo walionesha furaha na shukrani kwa TEKLA na serikali kwa kutambua kundi hilo, wakisema kuwa msaada huo umeleta faraja na thamani katika maisha ya watoto wao.
Tukio hilo limefanyika katika viwanja vya Gymkhan, likihudhuriwa na viongozi wa serikali, wazazi na wadau mbalimbali wa ustawi wa jamii, ambapo vifaa vilivyogawiwa ni pamoja na baiskeli za miguu mitatu, vifaa vya shule, sabuni na mavazi, kwa watoto wenye ulemavu.

Shirika la TEKLA limeendelea kuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono makundi maalum kwa njia ya misaada, elimu na uhamasishaji wa kijamii.
Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika mwaka huu yamebeba kaulimbiu ya kuhimiza usawa, ulinzi na fursa kwa watoto wote – ikiwemo wenye ulemavu.