Categories

Do you have a Story?

Call us on 0677 644 444 to submit your news story or incident report!

RC Macha:Wakuu wa Taasisi,Maafisa Habari,Mawasiliano Wajifunze Lugha ya Alama

Na Eunice Kanumba,Shinyanga

Wakati Shamra shamra za maadhimisho ya wiki ya viziwi  kitaifa  zikiwa yanaendelea katika mkoa wa Shinyanga,  mkuu wa mkoa huo Anamringi Macha  amewaagiza Wakurugenzi wa halimashauri zote za mkoa huo pamoja  na Wakuu wa Taasisi  kuhakikisha  maafisa Habari, na  Mawasiliano, wanapatiwa  mafunzo ya lugha ya alama ili waweze kusaidia mawasiliano katika utoaji wa huduma kwa  makundi maalum.

RC Macha ametoa agizo hilo wakati  akifungua Maadhimisho ya  Wiki ya Viziwi Duniani ambayo yalianza tarehe 23 Septemba, 2024  yanayotarajiwa kuhitimishwa September 28 huku  akisisitiza kuwa lugha ya alama ni sawa na  lugha nyingine zinazotambulika kimatifa.

“Nawaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri na Taasisi zote ndani ya Mkoa huu kuhakikisha wanawapeleka mafunzoni Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano ili waweze kusaidia mawasiliano na utoaji wa huduma kwa wananchi na hasa makundi maalum wakiwemo viziwi kwani hawa ni wenzetu na wanazo haki zote kama binadamu wengine,” amesema RC Macha”

Kwa upande wake katibu Tawala mkoa wa Shinyanga CP. Salum  Hamduni ameelezea utaratibu na ratiba ya  maadhimisho hayo  kuwa  yameanza tangu  tarehe 23 Septemba, 2024 na yatahitimishwa rasmi tarehe 28 Septemba, 2024 ambapo yanatarajiwa kufungwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete.

Awali akitoa salamu za Chama cha Viziwi Tanzania Mwenyekiti  mwenyekiti wa chama hicho  Celina Mlemba amesema kuwa, maadhimisho haya ni utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa la tarehe 9 Disemba, 1917 la kuzitaka nchi wanachama kufanya maadhimisho ya Wiki ya Viziwi Duniani kila ifikapo wiki ya mwisho wa mwezi Septemba ya kila mwaka ambapo kauli mbiu kwa mwahuu inasema “ungana kutetea haki ya lugha za alama”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *