Watu kumi na tatu wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja kwa tuhuma za kuhusishwa kufanya vitendo vya udhalilishaji kwa watoto watatu Zanzibar.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP. Richard Mchomvu amesema jeshi la Polisi limefanya operesheni kufatia video iliyokuwa ikitembea kupitia vyombo vya habari watoto wakieleza kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji na hivyo kuwahoji watoto hao na kutoa orodha ya watendaji wa makosa hayo.
Aidha Kamanda Mchomvu amekana kuwepo kwa mtandao rasmi wa wafanyaji wa matukio hayo, huku akieleza kuwa matukio hayo huchangiwa na kuporomoka kwa maadili ya watoto hao kwa kukosa malezi ya wazazi wawili.
Aidha amesema hadi sasa uchunguzi unaendelea na kesi tatu tayari zinaanza kusikilizwa mahakamani huku nyengine zikiendelea kufanyiwa uchunguzi