Mkuregenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Mohamed Janabi amesema, Serikali kupitia Hospitali ya Taifa Muhimbili imenunua vifaa vitavyotumika upandikizaji mimba/ujauzito (IVF clinic).
Amesema, tayari Hospitali hiyo imemaliza ujenzi wa jengo ambalo vifaa hivyo vitasimikwa ili wananchi wenye uhitaji wa huduma hizo waanze kunufaika.
Prof. Janabi amesema hayo wakati akitoa taarifa ya mafanikio ya Hospitali ya Taifa Muhimbili na mipango yake, katika ofisi za habari maelezo Jijini Dodoma.