WFP YAIKABIDHI SERIKALI KITUO CHA MKAKATI CHA ISAKA.

NA EUNICE KANUMBA

Shirika   la Mpango wa Chakula Duniani  (WFP) limekabidhi   kwa serikali ya Tanzania kituo cha Kimkakati kilichokuwa katika bandari ya nchi kavu  Isaka  wilaya Kahama mkoani  Shinyanga   lengo likiwa ni kugawa misaada ya chakula kwa wakimbizi waliokuwa wakitokea katika nchi za ukanda wa maziwa makuu  kufuatia machafuko  mbalimbali yaliyopelekea vita katika nchi za  Burundi na Rwanda katika mwaka 1994.

Kituo hicho chenye  eneo lenye ukubwa wa  Mita za Mraba 29450  serikali iliwapatia  WFP  tangu Januari  mwaka 1996  na mwaka 2004 ilithibitisha kwa barua kupokea kwake na mwaka 2024 imekabidhi kwa kurudisha rasmi eneo hilo kwa serikali.

 Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya eneo hilo Naibu  Mkurugenzi wa  Shirika la Chakula duniani  Christine Mendes  amesema kituo hicho cha Isaka kilijengwa na shirika hilo kwa madhumumuni ya kusambaza chakula cha msaada kwa wakimbizi ambapo chakula hicho kilikuwa kikisafirishwa kutoka bandari ya Dar es salaam  kupitia reli ya kati  mpaka katika kituo hicho.

Mendes alisema chakula walichokuwa wakisambaza zaidi ni Maharage,Mahindi na Mtama na  kwa kupitia na kupeleka kwenye nchi za  Rwanda,Burundi,Kongo, Kenya ,Sudani Kusini  na Uganda.

“Kituo hicho kilijengwa bure na WFP na kuweka mtandao wa miundombinu ya reli mbili za kutoka Stesheni ya Isaka  hadi kwenye kambi hiyo yenye umbali wa mita 1200  waliweka  Maghala 54 ya kuhamishika ,uzio,nyumba mbili za watumishi na Mashine “amesema   Mendes.

 Aidha Mendes ametoa   mapendekezo kuwa  eneo hilo wapatiwe  Shirika la  Reli (TRC) kwani shughuli walizokuwa wakizifanya  wao zinaendana katika kutunza mizigo na usafirishaji.

 Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa shirika la reli Tanzania Meneja wa Shirika  hilo kanda ya Tabora John Mamuya amesema wanashauri  eneo hilo  wapatiwe  wao kwasababu hata katika ujenzi wa Reli ya kisasa (SGR) watalitumia kuhifadhi vifaa na ujenzi huo utakapokamilika litatumika  kuweka mizigo inayotarajiwa kusafirishwa.

Naye Diwani wa kata ya Isaka  Pazi Majuta amesema  asilimia 70 ya uchumi wa Isaka ulijengwa na WFP na wao  walikaa kwenye Halmashauri na kujadiliana kuhusu eneo hilo  walipendekeza lilirudi kwenye kijiji  ili waweze kuendeleza eneo hilo kwa kuweka miundombinu kama shule au kugawa maeneo.

 Akitolea ufafanuzi  mapendekezo ya wadau hao Katibu tawala wilaya ya Kahama  Mohamed Mbega amesema ndio kwanza wamekabidhiwa eneo hilo  hivyo mapendekezo yote yatajadiliwa katika vikao husika .

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *