Wizara ya Fedha, imeutaarifu umma kuwa kujiepusha na matapeli kwani hakuna zoezi lolote la uhakiki wa mafao linalofanywa na Hazina.
Taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha imearifu kuwa katika siku za hivi karibuni kumeibuka wimbi la jumbe fupi za maandishi kwamba wahusika wapige simu ili kupewa taarifa zaidi kitu ambacho si cha kweli.



