Wanawake waandamana kupinga machafuko Congo

Mamia ya wanawake waliovalia wameandamana katika mitaa ya mji wa Kinshasa, wakishinikiza kukomeshwa kwa vita katika eneo la Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Maandamano hayo yaliyoitishwa na waziri wa jinsia, familia na watoto Mireille Masangu yaliwakusanya pamoja wanasiasa na watumishi wa umma, ambapo Waandamanaji walibeba mabango yaliyo na ujumbe uliosema : “wahanga milioni 12 tangu 1994, waoneeni huruma wanawake na familia mashariki mwa Kongo”, “Kongo itabaki moja na isiyogawanyika”.

Maandamano hayo yaliishia katika ofisi ya rais, ambapo waziri Masangu alitoa taarifa ya kulaani “matakwa ya upanuzi wa Rwanda na unyonyaji wa rasilimali za Kongo.”

Waziri huyo alishutumu kile alichokitaja kuwa ni ukimya, ushirikiano wa jumuiya ya kimataifa inayowakilishwa na Marekani, Ufaransa, Ubelgiji, Uingereza na Poland na sera yake mbaya ya kuunga mkono wavamizi wa Kongo na kwa upande mwingine namna isiyofaa katika kushughulikia misaada ya kibinadamu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *