Na Afarah Suleiman, Babati -Manyara.
Mkuu wa Mkoa Manyara, Queen Sendiga ametoa wito kwa Wanawake na jamii kwa ujumla Mkoani humo, kushirikiana kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia ambavyo vimekithiri Mkoani humo.
Wito huo ameutoa wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 49 ya kuzaliwa kwa chama cha mapinduzi ccm,yaliyo anadaliwa na jumuiya umoja wa wanawake ccm Mkoa wa Manyara UWT ambapo amesema kesi zaidi ya 800 zimeripotiwa katika kipindi hiki cha miaka mitano.

Jumuiya ya umoja wa wanawake wa Chama cha Mapinduzi – UWT Mkoa wa Manyara, imeadhimisha miaka 49 ya kuzaliwa kwa chama hicho, kwa kutoa misaada mbalimbali kwa watoto wenye mahitaji maalum, katika mji wa Magumu wilayani Babati.
kilele cha maadhimisho ya miaka 49 ya kuzaliwa kwa ccm ni Februari 5,Ambapo kwa mwaka huu kimkoa itafanyika Wilayani Hanang.