Wananchi, Yanga SC ni mabingwa wa Mapinduzi Cup, baada ya kuifunga Azam FC kwa mikwaju ya penalti 5–4, kufuatia sare tasa katika muda wa kawaida na nyongeza wa mchezo huo wa fainali.

Ndani ya dakika 90 mchezo ulimalizika kwa sare ya 0-0, kisha dakika 30 za nyongeza hakuna timu iliyofanikiwa kupata bao, huku yanga wakishindwa kuitendea haki nafasi ya mkwaju wa penati iliyopigwa na Pacome Zouzoua.
Dkk 90: Yanga 0-0 Azam
Dkk 30: Yanga 0-0 Azam
Penati: Yanga 5-4 Azam


