Staa wa muziki, Jux ameweka wazi video ya ENJOY imerejea kwenye akaunti yake ya YouTube. Ngoma hiyo amefanya na Diamond Platnumz ila wiki kadhaa msanii wa muziki kutoka Congo, Sapologuano aliripoti YouTube iondolewa kwa kile alichodai ameibiwa melody za wimbo wake wa I fond Love.
Mpaka sasa video hiyo inawatazamaji Milioni 16 YouTube huku TikTok ilifikisha Bilioni moja.Video hiyo imeongozwa na @fole_x, huku S2kizzy akiwa ndio producer.
