Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetozwa faini ya Sh25 milioni kutokana na uvunjaji wa maadili uliofanywa na kocha wa timu ya Taifa ya Tanzania, Adel Amrouche hivi karibuni, uliosababisha kocha huyo apewe adhabu ya kufungiwa mechi nane.
TFF imetozwa faini kutokana na kuvunja kanuni ya 110 ya fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) inayotaka timu shiriki kudhibiti mwenendo wa ofisa/maofisa wake.