Ni Toleo la 61 la Tamasha la Kimataifa la Uvuvi na Utamaduni la Argungu lililofanyika huko Argungu, Jimbo la Kebbi, Nchini Nigeria.
Tamasha hili limeonesha urithi wa kitamaduni wa Nigeria kupitia mashindano ya jadi ya uvuvi, muziki, densi, na maonyesho ya ufundi wa ndani.

Hili ni Tukio la kila mwaka, linaloshikiliwa na ukingo wa kihistoria wa mto wa Matan Fada (unaotambuliwa na UNESCO kama Turathi za Kitamaduni Zisizogusika za Binadamu), huvutia washiriki kutoka kote Nigeria na kwingineko.
Hata hivyo, Tamasha la mwaka huu, linakuwa la 61 tangu kuanzishwa kwake, limevuta umati mkubwa wa watu ndani na kutoka sehemu zingine za nchi hiyo.

Tukio hili ni maarufu likiwahusisha wavuvi wengi ambapo mamia ya wanaume hushindana, ili kuvua samaki mkubwa zaidi pamoja na maonesho ya kitamaduni, mieleka, maandamano ya durbar na maonesho ya kuadhimisha historia na mila za Kebbi.



