TAMASHA LA JADI LA BUSIA LAZINDULIWA RASMI SHINYANGA.

NA  EUNICE KANUMBA –UKENYENGE KISHAPU

TAMASHA la jadi  ambalo hufanyika kila mwaka kwa kuwakutanisha wanajamii katika himaya ya utawala wa Busiha linalojulikana kama sanjo ya Busia limezinduliwa rasimi kwa mwaka huu 2025  na kiongozi wa himaya hiyo chifu Makwaia wa tatu katika makazi yake yaliyopo kata ya Ukenyenge halimashuri ya wilaya ya Kishapu,mkoani Shinyanga.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Tamasha  hilo chifu Makwaia wa tatu ambaye ni kiongozi wa 24 wa himaya hiyo  ameitaka jamii ya wasukuma   kujivunia mila, desturi na tamaduni zao ambazo zmerithiwa kutoka kwa mababu kama sehemu ya kuzienzi na kuacha alama kwa vizazi vijavyo, na kwamba mila hizo hazipaswi kupuuzwa kwani hazajachakachuliwa kwa kuchanganywa na tamaduni za kigeni.

Kwa upande wao Washiriki wa tamasha hilo kutoka vikundi mbalimbali vya ngoma za asili ya Kisukuma wameeleza tija ya uwepo wa matamasha hayo hususani kutunza mila la tamaduni zilizoachwa na mababu na kujikwamua kiuchumia kupitia michezo wanayoshiriki.

Waratibu  wa tamasha hilo na shuguli za utemi  wa Busiya wamesema matamasha hayo yamekuwa yakisaidia kuwaunganisha jamii ya wasukuma kupitia michezo mbalimbali ambayo imekuwa ikijumuishwa katika tamasha hilo linalofanyika kwa mwaka wa 16 mfululizo

Tamasha hilo  la kitamaduni limekuwa likitumika kama jukwaa la kuonyesha utamaduni wa msukuma kwa shuguli zinazofanywa  ikiwemo Ngoma, mavazi ya asili ,michezo ya asili  vyakula vya asili huku shughuli hizo zikitarajiwa kuhitimishwa kesho  July 7 2025  katika viwanja vya  makazi ya chifu wa busiya.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *