Wizara ya Afya Nchini, imetoa tahadhari kuhusu ongezeko la visa vya magonjwa ya mfumo wa kupumua kama maambukizi ya mafua makali, kipindupindu na UVIKO -19.
Kwa mujibubwa taarifa iliyotolewa hii leo Februari 25 jijini Dodoma na Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Maghembe imeeleza kuwa, magonjwa huibuka kipindi cha Novemba na Aprili.

Amesema, magonjwa yote huambukizwa kupitia njia ya kukohoa, kupiga chafya au kuzungumza, na kwa kugusa sehemu zilizochafuliwa.