“Sitaki mtoto wa haramu” -Baba wa Mohbad

Baba mzazi wa marehemu Mohbad, Mzee Joseph Aloba, amejitokeza na kuomba kusaidiwa gharama ya kipimo cha DNA ili kujua baba halisi wa Liam (Mtoto wa Mohbad), kwani hataki kupokea mtoto haramu.

Bw. Aloba alitoa wito kauli hiyo katika mahojiano ya tarehe 24, Novemba, aliyofanya na Ibadan Oriyomi Hamzat.


“Nawaomba Wanigeria ambao wanapigania haki kwa Mohbad wasichoke, tafadhali naombeni mniunge mkono kwa sababu siwezi kufanya hivyo peke yangu.

Akaongeza “Naomba wanisaidie kujua nini kilimuua mwanangu. Na pia nataka DNA ya mtoto wake ifanyike kwa sababu sitaki kumkubali mtoto wa haramu”.

“Nahitaji msaada. Unajua kama baba, lazima nipange pesa kwa ajili ya DNA, na ninataka DNA ifanyike katika sehemu mbili tofauti. Nimezungumza na wakili wangu,” alisisitiza.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *