SIMULIZI YA FAMILIA MOJA YA WATU SITA ILIVYONUSURIKA KIFO SHINYANGA.

NA EUNICE KANUMBA –SHINYANGA 

Gari aina ya Toyota Harrier lenye namba za usajili T 223 DQR lililokuwa likitokea Dar kwenda Mwanza lllililobeba watu sita wa familia moja limeacha njia na kupinduka na kisha kutumbukia katika mtaro.

Tukio hilo limetokea Desemba 20, 2024  majira ya saa tisa alasiri katika eneo la kizumbi, Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga huku mmoja wa manusura wa ajali hiyo Diana Willbard (25) akielezea namna tukio hilo lilivyotokea.

“Tulikua tunatoka Dar kwenda Mwanza tulivyofika Tinde gari likapata shida likagoma kwenda, mjomba akaomba gari aina ya Noah wakaunganisha mabomba ya gari litusogeze mjini kwa ajili ya matengenezo lakini  tulivyofika hapa bomba la gari likaachia na kupinduka kwenye mtaro” amesema Diana.

Shuhuda wa tukio hilo Shija Mwandu amesema kuwa aliona gari ya abiria aina ya Noah ikiwa inavuta gari hili ghafla likaachia na gari ya nyuma ikapinduka kwenye mtaro.

“Gari ya abiria aina ya Noah lenye nambari za usajili T 885 CQG lenye kufanya  safari zake Tinde hadi Shinyanga mjini lilikuwa linavuta gari aina ya Toyota Harrier lkn ghafla Bomba likaachia na hii Harrier ikapinduka kwenye mtaro” amesema Shija Mwandu

Jambo media imemtafuta Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga  kamishina mwandamizi msaidizi wa jeshi la polisi SACP Janeth Magomi kuhusiana na tukio hilo ambapo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akiwataka madereva kuwa makini wawapo barabarani hususani katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *