SERIKALI YAHIMIZA MATUMIZI YA NDEGE NYUKI KATIKA KILIMO CHA PAMBA.

NA EUNICE KANUMBA-SHINYANGA

Matumizi ya teknolojia ya kisasa ya kutumia Ndege Nyuki (Drone) kunyunyizia dawa za kuuwa wadudu kwenye zao la pamba imeondoa adha kwa wakulima kutumia muda mrefu kufanya kazi hiyo.

Hayo yamebainishwa na wakulima wa zao la pamba katika Kijiji cha Kinampanda na Mwamalasa Katika  ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Anamringi Macha ya  kukagua maendeleo ya zao hilo na kusisitiza umuhimu wa kunyunyizia dawa za kuuwa wadudu.

Ngusa Mayunga mkulima katika Kijiji cha Mwamalasa Wilayani Kishapu Mkoa wa Shinyanga,amesema amelima  ekari kumi chini ya usimamizi wa wataalamu wa kilimo nakufuata kanuni bora ya ulimaji wa zao hilo kwa kuepuka kuchanganya na  mazao mengine ili kuwa na mafanikio makubwa.

Mayunga amesema  kipindi hiki nichakunyunyuzia dawa na kwamba   amekuwa akitumia pampu kwa kuibeba mgongoni  wakati mwingine anachoka nakutumia muda wa siku mbili au tatu kukamilisha shamba ekari moja ambapo kwa ndege nyuki inatumia dakika sita kwa ekari.

Mkulima mwingine Muhoja Peter mkazi wa Kijiji cha Kinampanda, amesema kunyunyizia dawa ya kuuwa wadudu kwenye pamba kwa kutumia pampu ya mkono ni changamoto kubwa kwani wanatumia nguvu kubwa ambapo kwa sasa uwepo wa ndege nyuki umelahisisha kazi.

Kwa upande wake Mkuu  wa mkoa wa Shinyanga  Anamringi Macha amesema kitaalamu  Teknolojia hiyo ya kutumia drone ikisetiwa vizuri  inauwezo wa kunyunyizia  ekari moja kwa dakika  sita na kuwataka wakulima kuitumia ili kuongeza idadi ya kilo wanazozalisha.

‘Tunataka uzalishaji wa zao la pamba kwa ekari moja ufikie kilo 1200 ili kuleta tija kwa mkulima,ambapo kwa sasa wakulima wengi wanapata kilo 250 hadi 300 tunataka tutoke huko na ndiyo maana serikali imekuja na teknolojia ya kisasa ya kutumia ndege nyuki”amesema  Macha

Msimamizi  wa  zao la pamba  kutoka  Bodi ya pamba  Wilayani Kishapu   Thadeo  Mihayo amesema  kwa mkoa wa Shinyanga zipo drone saba  lakini mipango iliyopo ni kuongeza  zingine ili kufikia  drone 14.

Mihayo amesema matarajio ya  kulima zao la pamba  kwa Wilaya ya Kishapu kwa msimu wa mwaka  2024/2025  ni ekari  220,000  na kwamba  bodi ya pamba iko tayari na inaendelea kusimamia  zao hilo kwa umakini.

Ofisa kilimo  kupitia mradi wa jenga  kesho iliyobora (BBT) Yombi Chedi  amesema  changamoto iliyokuwepo kwa wakulima  wa kata ya Mwamalasa  ni kukosa elimu ya kilimo bora kwani walio wengi walikuwa wakichanganya zao la pamba na mazao mengine.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *