Wasanii wawili na maarufu kutoka Tanzania maarufu kama ‘The Ramadhani Brothers’ wametua Dar es salaam na kupokelewa na Viongozi mbalimbali wa serikali hii ni baada ya Kurejea Kutoka Marekani walipokuwa wameenda kushiriki katika shindano la kusaka vipaji la America’s Got Talent (AGT) Fantasy Legue na kuibuka na ushindi dola 250,000 za Kimarekani (zaidi ya Milioni 600 za Kitanzania)
Mapokezi hayo yameongozwa na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) chini ya Katibu Mtendaji wa BASATA Dkt. Kedmon Mapana na Viongozi wengine wa Serikali.