Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa fedha kiasi cha Sh/= Bilioni 9 kwa ajili ya kusomesha wataalam bingwa na bobezi 601 fani mbalimbali za afya ili kuongeza idadi ya wataalam wenye ujuzi wa kutoa huduma za kibingwa hapa nchini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu leo hii Novemba 29, 2023 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Mpango wa Rais Samia Suluhu Hassan wa kuongeza wataalam bingwa na bobezi wa afya nchini kwa mwaka wa fedha 2023/24.
Waziri Ummy amesema fedha hizo zitatumika kugharamia mafunzo kwa wataalamu wapya 601 sawa na 92% ya waombaji ambao walikidhi vigezo vya kusomea utaalamu wa ubingwa na bobezi wa fani mbalimbali za Sekta ya Afya.
Aidha, Waziri Ummy amewataka wataalamu wote waliopata ufadhili huu wa mwaka 2023/2024 kukamilisha taratibu za kujaza mikataba ya ufadhili kama ishara ya kukubali ufadhili huu


