NGATALE ACHUKUA FOMU UBUNGE SHINYANGA MJINI.

NA EUNICE KANUMBA, SHINYANGA 

LEO ikiwa ni siku ya tatu  tangu kufunguliwa kwa zoezi la uchukuaji fomu kwa watia nia, Aliyekuwa mkurugenzi msaidizi idara ya sheria katika Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI) Eustard Ngatale leo ametia nia ya kugombea ubunge jimbo la Shinyanga mjini kwa kuchukua fomu  katika ofisi za chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Shinyanga mjini.

Ngatale amekabidhiwa fomu hiyo leo majira ya saa tatu asubuhi na katibu wa CCM wa wilaya ya Shinyanga mjini Ndugu Hamisa Chacha. 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *