
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI imejengewa uwezo kuhusu Mpango wa DREAMS unaotekelezwa na Mradi wa EPIC ambapo mpango huo unalenga katika kupunguza kiwango cha maambukizi ya VVU miongoni mwa wasichana balehe na wanawake vijana.
Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mpango huo katika semina ya Kamati hiyo Bungeni Jijini Dodoma Mratibu wa Mpango wa DREAMS Mkoa wa Shinyanga Bi. Agness Tunga amesema Mradi wa EpiC unalenga makundi maalumu na anayohitaji kupewa kipaumbele ikiwemo wasichana wa rika balehe na kina mama vijana, na wanaume na wanawake walio katika hatari ya kupata maambukizi ya VVU.
Amesema mradi unatekelezwa katika Mikoa 11 Mradi wa EpiC ulianza utekelezaji wa mpango wa DREAMS katika ngazi ya jamii mnamo Februari 2020 kwa Mabinti wa rika balehe (15-19) na Wakina Mama vijana wenye umri kuanzia miaka (20-24).