Staa muziki, Mr Eazi amefunga ndoa ya siri na binti wa Bilionea Nigeria, Temi Otedola.
Katika mahojiano aliyofanya na kituo cha Naija 102.7 FM, hivi karibuni. Mkali huyo alijikuta akipata kigugumizi baada ya kuulizwa juu ya Maisha yake ya ndoa yapoje?! na kwanini hakualika watu?
“Nashukuru Mungu yapo safi, ila nani anasema sikuwaambia kuwa nafunga ndoa?!…. ilikuwa ndoa ya kifamilia zaidi” amesema Eazi.
Aprili 2022 Mr Eazi alivalisha pete ya uchumba binti huyo, baada ya kuwa kwenye mahusiano kwa takribani miaka mitatu.



