Mohbad alikuwa na shoo Canada

Promoto wa shoo huko nchini Canada, Prince George, ameweka wazi kuwa msanii Mohbad alikuwa na shoo nchini humo, na visa yake ilikubalika siku aliyokufa.

George alisema hayo alipokuwa kwenye maandamano ya kuwasha mishumaa ya maomboleza yaliyoandaliwa na Wanaijeria mjini Toronto, Canada Jumamosi usiku.

“Nilituma ujumbe kwa meneja wa Mohbad asubuhi ya siku aliyofariki ili kumjulisha kwamba visa yake ilikuwa imeidhinishwa, daah imeniuma sana maana niliambiwa kuwa Mohbad amefariki,”anasema promota huyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *