
Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amesema ujenzi wa jengo la kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi utaanza kutekelezwa katika mwaka wa 2023/2024 na kukamilishwa mwaka wa fedha 2024/2025 ambapo kiasi cha shilingi milioni 300 kimetengwa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa jengo hilo.
Dkt. Mollel ameyasema hayo leo Mei 6,2024 Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mhe. Taska Mbogo Mbunge wa Viti Maalum aliyetaka kujua ni lini Serikali itajenga jengo la kuhifadhia Maiti Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Katavi.
Amesema katika kipindi cha mwaka 2021 hadi 2024 Serikali imetoa fedha kiasi cha shilingi Bilioni 12.9 kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi.


