Dada wa msanii wa muziki Mimi Mars Vanessa Mdee kupitia ukurasa wake wa Instagram ametoa taarifa ya kiafya ya mdogo wake ambaye alipata ajali ya gari siku kadhaa zilizopita ambapo amebainisha anaendelea vyema.

“Mimi Mars anaendelea vizuri kwa sasa na familia ingeomba kupewa faragha katika kipindi hiki”, ameandika Vanessa.
