“Madhara haya yaliyotokana na janga hilo [maporomoko Hanang] hadi sasa yamesababisha vifo 76 mpaka leo, majeruhi 117 na kaya 1,150 zenye wakazi wapatao 5,600 zimeathirika. Ekari 750 za mashamba zimeharibika, na pia kuna vifo vya mifugo” amesema Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama.
