KITUMBO ACHUKUA NA KURUDISHA FOMU KATA YA MJINI.

NA EUNICE KANUMBA –SHINYANGA 

KADA maarufu wa chama cha mapinduzi Salum Kitumbo  amechukua na kurudisha fomu akitia nia kugombea udiwani wa kata ya mjini kwenye manispaa ya Shinyanga. 

Kitumbo mweye elimu ya shahada ya kwanza ya bishara na utawala kutoka chuo kikuu cha  Dar es salaam lakini pia mwenye taaluma mbalimbali katika nafasi za uongozi  huku akifanya kazi katika kada ya biashara  ambapo amekuwa mshauri wa kibiashara  wa kampuni ya jambo group of companies. 

Kitumbo anatajwa kuwa ni miongoni mwa Wanachama wa muda mrefu wa Chama cha mapinduzi huku ikitajwa kuwa alijiunga na chama hiko tangu mwaka 1984.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *