
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza uchaguzi mdogo wa madiwani kwenye kata 23 za Tanzania Bara utakaofanyika Machi 20, mwaka huu.
Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Tume hiyo, Kailima Ramadhani imesema tume imepokea taarifa kutoka kwa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa kuhusu uwepo wa nafasi wazi za madiwani katika kata hizo, taarifa iliyozingatia matakwa ya kifungu cha 13(1) na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292.
Aidha imeeleza kuwa fomu za uteuzi zitatolewa kuanzia Februari 26 hadi Machi 04, mwaka huu ambapo uteuzi wa wagombea utafanyika Machi 04, 2024 na kampeni za uchaguzi zitafanyika kuanzia Machi 05 hadi 19, mwaka huu.