Jua Cali atoa neno kwa Wasanii wa Bongo, amtaja Diamond na Alikiba

Msanii mkongwe wa muziki kutoka nchini Kenya, Jua Cali, amedai kuwa wasanii wa Tanzania wanafanya shoo sana Kenya kwa sababu Kenya kuna pesa nyingi kuliko Tanzania.

Jua cali amesema hayo kupitia mahojiano aliyofanya na waandishi wa habari hivi karibuni.

Mkongwe huyo pia akaongeza kuwa Kenya wasanii zaidi ya 15 wanafanya Shoo ndani na nje ya nchi, lakini Tanzania ni wasanii wawili tu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *