Staa wa muziki, Harmonize amerudisha shukrani kwa Rayvanny kwa kutoa baraka kwenye kazi yake mpya ya 54U inayojumuisha ngoma zipatazo sita.

Ngoma hizo zimetoka sita, siku ya juzi usiku na kuna ngoma kama’ Wababa’, ‘My Lady’, ‘Mi Amor’, ‘Kitu Kizito’ ambayo amemshirikisha Missi Misondo, kuna ‘Money’ na ‘ Christmass’.
Utakumbuka pia wakati Harmonize ametoa Albamu yake ya ‘Visit Bongo’, Rayvanny pia alionyesha kuisapoti kwa kupost kwenye Insta Story yake.