Hawa Nitareja apata mtoto atoa neno kwa ‘SIMBA’

Akufaye kwa dhiki ndio Rafiki.. kwa kudhililisha Hilo Hawa Ramadhan maarufu kama Hawa Nitarejea ametoa shukurani zake kwa msanii wa muziki Diamond Platnumz ambaye alimsaidia mwaka 2018 kwa kumfanya aweze kutibiwa wakati huo ambapo alikuwa anahitaji kufanyiwa upasuaji wa moyo.

Hawa amebainisha hayo kwa kuweka wazi kupata mtoto wa kike hivi karibuni.” Alhamdulillah napata muda WA kushukuru Nimekumbuka nilikotoka haikuwa rahisi na sikuwaza mwannzo kama nntaitwa tena MAMA, Ila #diamondplatnumz MUNGU akubariki Sana akuzidishie palipopungua mashaallah Una moyo ambayo sijui kuufananisha katika Maisha yangu ulinikomboa pakubwa Alhamdulillah 🙏, Sio tena NASIB nimepata binnti anaitwa MARIAM Alhamdulillah, Nawashukuru watannzania wote Kwa upendo wenu WA Hali na mali kwangu nguvu zenu ni kubwa nawapenda Sana MUNGU awabariki innsha’Allah🤲.”

See translation

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *