Klabu ya soka ya Geita Gold FC imetangaza kufikia maridhiano ya kusitisha mkataba na Kocha Hemedi Suleiman Morocco.

Klabu hiyo imesema imeridhia ombi la kocha Morocco kusitisha mkataba kwa sababu alizozitaja kocha huyo ikiwa ni pamoja na kubanwa na majukumu ya timu ya Taifa.
Aidha klabu hiyo imemshukuru kocha Morocco kwa kipindi chote alichohudumu kama kocha wao mkuu.
Inaelezwa siku yoyote kutoka leo klabu hiyo itamtangaza aliyekuwa kocha wa Namungo FC, Denis Kitambi ili kuchukua nafasi ya Kocha Morocco


