DC SHINYANGA AMTAKA MKURUGENZI KUSHUGHULIKIA HOJA 50 ZA CAG.

NA EUNICE KANUMBA –SHINYANGA 

MKUU wa wilaya ya Shinyanga wakili Julius Mtatiro  ametoa maagizo kwa mkurugenzi mtendaji wa halimashauri ya wilaya ya Shinyanga Dr. Kalekwa Kasanga kushughulikia  Hoja 50 zilizoibuliwa katika ripoti iliyopita  ya   mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali (CAG) ambazo bado utekelezaji wake unaendelea na kwamba  vipatikane vielelezo vyenye majawabu ya   hoja hizo hadi  ifikapo tarehe 18 june 2025 ili hoja hizo ziweze kufungwa kwa mujibu wa taratibu.

Wakili Mtatiro amebainisha hayo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga Anamringi Macha leo Juni 11, 2025 wakati akihutubia baraza maalum la madiwani  lililoketi kupitia taarifa ya mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali (CAG) zilizokaguliwa katika mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2024.

Awali akisoma hoja hizo  zilizoibuliwa na katika ripoti ya CAG mkurugenzi mtendaji wa halimashauri ya wilaya ya Shinyanga Dr. Kalekwa Kasanga amesema halmashauri hiyo ilipata hati safi  katika hesabu za mwaka wa fedha 2023/2024 huku akianisha kuwa katika mwaka huo ziliibuliwa hoja 52 ambapo hoja mbili zimefungwa na kubaki hoja 50 ambazo bado utekelezaji wake unaendelea.

Aidha, Dr. Kasanga pia amehaidi kutekeleza maagizo yaliyotolewa  Dc Mtatiro na kwamba wanakwenda kutekeleza maagizo hayo ili ifikapo tarehe 18 june ili  hoja zenye uwezekano wa kufungwa ziweze kufanyiwa mchakato  wa kufungwa na kumalizika kabisa 

 “Mheshimiwa Mwenyekiti napenda kukutaarifu kwamba, kwa hesabu za mwaka wa fedha unaoishia tarehe 30 Juni 2024, Halmashauri yako imepata Hati Safi,” amesema Dk.Kasanga.

Akizungumza pia katika kikao hicho, Afisa kutoka ofisi ya  Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika Mkoa wa Shinyanga CPA Yusuph Mabwe, amesema kwamba utekelezaji wa mapendekezo ya hoja hizo kasi yake iongezeke sababu yanatekelezeka.

Katika hatua nyingine  Halamashuri hiyo ya wilaya ya Shinyanga sambamba na   kupata Hati Safi, lakini pia imevuka lengo la ukusanyaji wa mapato kwa kukusanya  asilimia 106 ya  mapato kwa mwaka wa fedha uliopita.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *