Davido aahidi kutoa Zaidi ya Mil.500 kusaidia Yatima nchini kwao

Staa wa muziki kutoka nchini Nigeria, Davido kwa kushirikiana na taasisi yake ya David Adeleke Foundation (DAF) wameahidi kutoa jumla ya Naira Milioni 300 ambazo ni sawa na Tsh/= 506,705,198.13 kwaajili ya kusaidia vituo vya Watoto yatima vilivyopo nchini Nigeria.

Davido ametoa taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa X na Instagram kwa kuandika “Mimi na taasisi yangu tunaahidi jumla ya Naira milioni 300 kwa vituo vya watoto yatima kote Nigeria … kama mchango wangu wa kila mwaka kwa Taifa ❤️ …

Davido ni miongoni mwa wasanii ambao mwezi huu wa Valentine ameonyesha upendo kwa kulibeba jambo la mtu mwingine kama lakwake na hii ndio maana halisi ya ‘Mimi ni Wewe’.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *