Rapa Cardi B amejitetea kitendo chake cha kumtwanga shabiki na microphone mwezi Julai wakati wa shoo yake huko Las Vegas na kubainisha kuwa hakukusudia kufanya hivyo.

Akizungumza wakati wa mahojiano kwenye The Breakfast Club, anafunguka kuwa alijikuta akifanya hivyo baada ya shabiki kumrushia maji ya barafu wakati wa onyesho lake, ndipo akapatwa na hali hiyo na alijua ataenda jela ila hakwenda.
Baada ya kampuni husika ya Mic hiyo kuipata mic yao wakaiingiza kwenye mnada ambapo ikauzwa kiasi cha Dola 100,000 ambazo zimetumika kusaidia wenye uhitaji jijini humo.