Charlene Ruto, binti wa rais wa Kenya,Willum Ruto ni miongoni mwa walioshiriki mkutano wa maombi ya kupata mume, maombi hayo yaliongozwa na mhubiri wa Marekani, Benny Hinn wikiendi iliyopita Jijini Nairobi Nchini Kenya.

Benny Hinn alimwombea apate mume atakayeweza kusapoti kazi zake, “Mpe mume ambaye atatimiza wito huo naye. Bwana mpeleke kijana huyo njia yake,”alisema muhubiri huyo
Rais Ruto, mke wa rais na Naibu Rais Gachagua walikuwepo huku Charlene akiomba maombi kwa ajili ya wito wake wa kuwasaidia vijana.