BILIONI 20 KUFIDIA WALIOPISHA UJENZI UWANJA WA NDEGE KIPUNGUNI

Serikali imetoa Bilioni 20 kwa ajili ya malipo ya fidia kwa wakazi zaidi ya 200 wa Kata kipunguni Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Haya yamebainishwa leo na Mkurugenzi mkuu wa Viwanja vya ndege nchini (TAA) Abdul Mombokaleo Jijini Dar es Salaam wakati wa Halfa ya makabiziiano ya fedha kwa wananchi wa kata hiyo ya Kipunguni ambapo amesema fidia hizo zitatoka kwa awamu mpaka kukamilisha idadi ya wakazi wa kata ya kipunguni 1864.

Mkurugenzi mkuu wa Viwanja vya ndege nchini (TAA) Abdul Mombokaleo, amesema lengo la serikali na mamlaka hiyo kila mkazi ambaye amefanyiwa uthamishaji atalipwa fidia na kila mmoja atapata haki yake ipasavyo kwani ni mali za wananchi na watapewa kwa wakati husika.

Kwa Upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Mkuu wa Fedha na Utawala kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini(TAA), Shadrack chilongani mchako wa kuwalipa wananchi utafanyika mara baada ya wao kujaza fomu ambazo zipo serikali ya mtaa wa kipunguni.

Naye Mbunge wa Jimbo la Segerea, Mhe. Bonnah Ladislaus Kamoli, ameipongeza Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri ya kuhakikisha wananchi wa kipunguni wanapata fidia ikisimamiwa na Mkurugenzi wa TAA kwa kuhakikisha wananchi hao wanalipwa fidia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *